Monday, June 18, 2012

Tusker Project Fame Yashutumiwa Kukosa Mvuto-Mshiriki wa Tanzania Atolewa


Jana mshiriki mwingine kutoka Tanzania, Imani, 30, alitolewa kwenye shindano la Tusker Project Fame na kuungana na mshiriki wa Sudan Kusini, Mer.
Hata hivyo uamuzi huo uliwachukiza watazamaji wengi ambao wanasema shindano hilo sasa limepoteza mvuto na linaendeshwa hovyo hovyo.
Jambo kubwa lililowachukiza watazamaji ni kitendo cha kumuokoamshiriki wa Kenya, Doreern ambaye wanasema hajui kuimba kuliko Imani na Mer waliotolewa.
“Why people save Doreen? sorry for Mary and Iman but that is competition lazima mshindi awe ni mmoja,” aliandika msichana aitwaye Shamila Omary kwenye Facebook.
“Msiwe na hasira! Walipewa ushindi ili muende mkapate Tusker kadhaa kwa bar – a fundraising strategy for next years TPF kitty.”aliandika Akula Akwabi kwa utani.
Baadhi ya watazamaji wamedai kuwa washiriki wa shindano la msimu huu hawana vipaji zaidi ya kushindania pesa tu.
“Aiiihh…..TPF 5 shud be converted to East African tusker music and drama festivals for novice and meanows…nkt,” aliandika James Kinyua. ‘It looks like a colorful performance on KBC education channel….bure kabisa…nimewacha kukunywa tusker I don wanna contribute to this non starters kitty..” aliongeza.
The tpf5 contestants r so boring,,,kwanza kenyan ladies,” alisema Jedidah Sonnie
source:bongoflavortz