Friday, November 29, 2013

Hermy B afunguka kuhusu uhusiano kati yake na AY na FA



  Hermy B afunguka kuhusu uhusiano kati yake na AY na FA,asema kazi zinakuja

Moja kati ya habari nzuri ambazo zimewasurprise watu wengi leo ni kuhusu kurudi kwa urafiki uliokuwa umevunjika kati ya Hermy B, AY na mwana FA. AY na FA wamempa kampani kubwa producer Hermy B kwenye birthday party yake iliyofanyika usiku wa kuamkia leo na kupost picha kwenye mitandao ya kijamii.

Tovuti ya Times Fm imefanya mahojiano na Hermy B ambaye tayari ameingia nchini Kenya kwa ajili ya kuendelea na majukumu yake ya ujaji kwenye shindano Tusker Project Fame huku akisherehekea siku yake ya kuzaliwa leo (November 29).

Akiongelea kuhusu uhusiano uliopo kati yake na maswahiba wawili kwenye muziki AY na FA ambao awali walitofautiana kikazi na kila mmoja kuendelea kivyake, Hermy B amesema yeye na wasanii hao walimaliza tofauti zao siku nyingi na wamekuwa wakiishi kama washkaji kwa muda mrefu japokuwa hawakuweka kwenye media.

“By the way mimi na AY na Mwana FA unajua tunakutana mara nyingi sana, yaani tunapokutana ni nje ya nyumbani kwangu ambapo utanikuta niko mimi, AY, Mwana FA, yupo Fid Q,  Salama unamkuta yuko pale. So, most of the time tuko pamoja, hii ni kitu tu tumewaonesha kwamba as much as watu walikuwa wanafikiria labda kuna kitu kinaendelea lakini hapana, sisi tuko peace long time tumeamua ku-reveal tu sasa hivi,”

“Kiukweli sisi ni washikaji ambao tuko tight sana, nafikiri jamii tu ndio inaelewa kivingine. Unajua watu wengi wanafikiri mkishindwa kuelewana kitu fulani basi hamuwezi kuelewana, hapana…kwa sababu imagine sisi kila siku jioni kabla sijaingia kwenye nyumba yangu kulala nakutana na AY tunakaa tunapiga story mpaka saa nane za usiku ndo kila mtu anaenda kwake kulala,” amefunguka Hermy B.
Amesema hivi karibuni alikuwa na AY Nairobi, na walikaa na Fid Q na Prezzo na kupiga story usiku wote hadi asubuhi.

Hermy ambaye ni producer na C.E.O wa B’Hits amezungumzia mpango wao wa kufanya kazi tena kama ilivyokuwa zamani.
“Kazi tutafanya, unajua hizi ni plans za mbeleni na tumekuwa tunaongea ni jinsi gani tunaweza tukafanya kazi vizuri na kwa faida zaidi na kila mtu awe na furaha moyoni mwake unajua. Kwa hiyo kazi zitakuja hatuwezi kuwaambia lini, kesho kutwa au mwezi ujao.”

Ladha ya ngoma kali zitakazopikwa tena kama ‘Habari Ndio Hiyo’ itawakusanya tena mashabiki wa B’Hits, AY na FA pamoja kwa ajili kuusapoti muziki mzuri. Lini hasa?

Ameeleza Hermy B, “time ikifika, the right time statement itatoka kwamba tunafanya nini pamoja au nini kinaendelea interm of kazi and then wale mashabiki wote ambao walikuwa wanatupenda watatujoin watuongezee nguvu sasa tuweze kuifikisha Tanzania ambapo inatakiwa ifike.”

Monday, November 25, 2013

WANITAMANI NDIO UJIO MPYA WA BELLE 9

Belle 9 kuachia wimbo mpya kesho, unaitwa 'Wanitamani', asema ameufanya kiafrika zaidi


Belle 9 toka Morogoro ambaye ni moja kati ya vocalists bora Tanzania ataachia ngoma mpya kesho (November 26), ngoma aliyoipa jina la ‘Wanitaka.’
Akiongea na DJ K U, Belle 9 amesema mdundo wa ngoma hiyo umefanywa na Producer wake aliyemtoa ‘Tris’ ambae hivi sasa yuko Afrika kusini kimasomo na kwamba vocal amefanya kwa producer Mona Gangster.
Akiongea na DJ K U, Mkali huyo wa ‘Listen Now’ amesema ngoma hiyo iko katika mahadhi ya kiafrika na inayochezeka na pia imebeba ujumbe wa mapenzi.
“Hiyo ngoma ni muziki flani hivi wa kiafrika kwa sababu sasa hivi African Music ndio muziki ambao umeiteka dunia nzima hata wasanii wa Afrika wanauza sana huko Ulaya. Watu wamezoea kunisikia sana kwenye beat za R&B sana, kwa hiyo round hii nimechange kidogo ili kutengeneza mazingira ya hata kupata nafasi sehemu za mbali.” Amefunguka Belle 9.
Alieleza pia kuhusu ujumbe alioujaza kwenye ‘Unanitaka’, “Ngoma inaelezea wanawake ambao wana-fake kwa sababu kwenye hali ya kawaida wasanii huwa tunasumbuliwa sana kwamba I love You, I love You, lakini ni kwa sababu tu we ni star.”

Sunday, November 24, 2013

ANGALIA PICHA ZA KWENYE SHOW YA P-SQUARE TISHA SANAAAAAA


Peter na Paul Okoye wa kundi la P-Square wakilivamia jukwaa la Leaders usiku huu.
Mashabiki wakipagawa na shoo ya P-Square.

Joh Makini akilitawala jukwaa.
Nikki wa Pili (kushoto) na G Nako wakifanya yao stejini.
Kundi la Weusi likiongozwa na Joh Makini likishambulia jukwaa la Leaders Club 
kabla P-Square
 hawajapanda usiku huu.

Mwanamuziki Joseph Haule 'Profesa Jay' akiwapagawisha vilivyo mashabiki
 waliohudhuria shoo ya P-Square Live in Dar ndani ya Viwanja vya Leaders Club 
vilivyopo Kinondoni jijini Dar.
Nyomi baada ya kuikubali vilivyo shoo ya Profesa Jay.

Mwanamuziki Judith Wambura 'Lady Jaydee' au 'Anaconda' 
akiwapagawisha mashabiki wake waliohudhuria katika Viwanja vya Leaders Club
 usiku huu katika shoo wa wakali P-Square.
Watu... Jideeeeeeeeeeee...
Machozi Band nao walikuwepo kumback up Jide.
Mwanamuziki Ben Pol akiwasha moto katika steji ndani ya Viwanja vya Leaders 
usiku huu katika shoo ya P-Square Live in Dar.
Nyomi ikifuatilia shoo ya Ben Pol.
Ben Pol akiimba sambamba na mwanadada.
picha kutoka GlobalPublishers

Friday, November 22, 2013

B'Hits yatoa ufafanuzi kuhusu kuwaondoa Mabeste, Vanessa na Gosby

Jana B’Hitz Music Group iliweka wazi uamuzi wa kuwaondoa kwenye label hiyo wasanii watatu ambao ni Vanessa Mdee, Mabeste na Gosby.

Japokuwa Vanessa na Mabeste walitangaza wiki hii kujitoa kwenye label hiyo, huku Gosby akiwa bado hajasema chochote, timu ya BHits imesema kuwa wasanii hao waliondolewa kwenye label hiyo miezi miwili iliyopita japokuwa hawaamua kutangaza.
Mabeste aliiambia Times fm kuwa ameamua kujiondoa katika label hiyo kwa kuwa muziki wake ulikuwa haumlipi na kwamba maisha aliyokuwa anaishi ndiyo yaliyopelekea yeye kudhaniwa kuwa anafanya show za nje, na kwamba amechoka kuwa mzigo kwao.
Tovuti ya Times fm ilimtafuta Amani Joachim ambaye ni mwana sheria na Chief Operations Officer wa B’Hits Music Group ili kufahamu kuhusu sababu alizozitoa Mabeste kwa upande wa B’Hits, na mikataba ikoje na kama watachukua hatua zozote za kisheria.
“Hiyo statement ambayo Mabeste ameamua kuisema kwangu mimi naona haiko sawa kabisa. Sisi ni ndugu na tulikuwa tunaishi hivyo, tatizo la mtu mmoja ni tatizo la mtu mwingine yaani tunakuwa pamoja kabisa. Na kuna vitu vingi ambavyo Mabeste anajua kwamba tunavifumbia macho. Hata hiyo mikataba, sisi na Mabeste kuna kipindi tume-deal hata bila mikataba na mambo yakawa safi tu kwa sababu kuna ile heshima na kuaminiana.” Amesema Amani.
Ameyaelezea pia madai ya Mabeste kuwa mabadiliko yake katika maisha ndiyo yaliyosababisha B’Hits kuhisi kwamba anapiga shows za nje.
“Mabeste inabidi aangalie statements zake, na muda ambao anaamua kutoa hizo kauli kwa sababu kati yetu sisi tuna siri nyingi sana (Mabeste na Upande wa B’Hits). Tusifike sehemu kwamba tukaanza kufaidisha kila mtu, hicho ndicho kitu ambacho ningependa kukiweka sawa. Hizo shows na vitu vingine ambavyo labda alikuwa anavifanya akiwa nje tunavifahamu vingi tu, lakini kutokana na ule u-brother na nini tunavichunia tu.” Ameeleza kiongozi huyo wa B Hits.
Hata hivyo Amani amekubaliana na kuwepo kwa ubovu wa soko la muziki ambapo amesema hata shows zikiwepo bado malipo yanayotolewa yako chini kiasi kwamba Kampuni haliwezi kuendeshwa kwa kutegemea kugawana kipato hicho na msanii.
Aliongelea pia madai ya Mabeste kuwa B’Hits haikuwa inamfanya atengeneze pesa kupitia muziki wake.
“Well, hopefully kule anakoenda atapata. Tunaelewa Mabeste ana majukumu, maisha yake tunajua kwamba yamebadilika kwa namna flani. Personally nafahamu, sijui akina Harmy na Pancho. That’s why I’m ready to stay quiet kwenye vitu kama hivyo, nilikuwa tayari kukaa kimya…sina haja ya kufunguka ni vitu vingapi ambavyo Mabeste ameshafanyiwa katika hali ya u-brother, I will not say them kwa sababu kipindi mimi navifanya nilivifanya katika good will na nilitaka iishie hivyo, Amani will never say them.”
Jana C.E.O B Hits Hermy B aliuambia mtandao wa Bongo5 kuwa Vanessa, Gosby na Mabeste hawana shukurani kwa kile ambacho B Hits imewafanyia na kutoa mfano kuwa alitoa shilingi million nane mfukoni kulipia video ya Closer ya Vanessa  na kiasi kingine kulipia kazi alizofanya nje ya studio za B Hits, fedha ambazo hazijawahi kurudi.
Nae Amani Joachim alitoa ushauri kwa Vanessa, Mabeste na Gosby kwa ujumla kuwa wawe na amani na waendelee kufanya mambo yao na kuacha kutengeneza vita kati yao na B’Hits kupitia media kwa kuwa hata yeye ameamua kuyafumbia macho mengi.  
Lakini vipi kuhusu hasara ambayo B’Hits itaipata kutokana na kuondoka kwa wasanii hao kwa kuwa walichukuliwa wakiwa hawana majina na wakati huu wanaondoka wakati wameanza kuwa productive.
Mwana sheria na Chief Operations Officer wa B’Hits anaeleza.
“They were real productive na naweza kukwambia kweli hawa watu wako very talented, na B’Hits haijawahi kum-house mtu ambaye ni mbovu, na ndo maana watu wanashangaa kwa nini mna nyumba kubwa ya media halafu mna watu watatu tu, sisi kuna kipindi tulikuwa na msanii mmoja tu Mabeste for like 4 years, ni kwa sababu tunaangalia talent.
“Na kusema kwamba sasa hivi tutakuwa hatujarudi nyuma utakuwa ni uongo, kuondoka kwao ndio tutarudi nyuma steps kadhaa, lakini pia kutokana kwamba plans tulizopanga kufanya wakati tukiwa nao zilikuwa hazijafika kuiva, we are ready to do that with someone else, Mungu hajagawa kipaji kwa watu wawili au watatu.”
Amesema anaamini baada ya Gosby, Vanessa, na Mabeste watakuja watu wengine ambao wana vipaji pia.
Kauli ambayo inaungana na ile ya Hermy B kuwa B’Hits itatangaza wasanii wapya wa label hiyo mwanzoni mwa mwaka ujao.
Tovuti ya Times fm ilitaka kufahamu kutoka kwa mwana sheria huyo kuhusu mkataba kati ya B’Hitz na wasanii hao na damages/athari za kuvunja mkataba huo zikoje na iwapo watawadai wasanii hao.
Amesema mikataba ilikuwa tight lakini kwa mazingira ya Tanzania na hali halisi ya kipato cha wasanii wa Tanzania hiyo mikataba inakuwa kama useless kwa kuwa kiasi kinachotakiwa kulipwa na msanii huyo ni kikubwa kuliko hali halisi ya maisha ya msanii husika.
“Ukimchukua bwana mti ukampeleka mahakamani, mahakama inaangalia damage ambayo imeingia katika kampuni, na mwisho wa siku inachukua maamuzi ambapo itakwambia bwana mti kama amepatikana na kosa amlipe bwana jose million 150 Kwa mfano, haimfungi. Problem ni kwamba bwana mti hana hata shilling 200 mfukoni mwake, we unadhani utamfanyaje bwana mti?” Alieleza kwa mfano.
“Kwa sababu mahakama ikishakupa judgement inakuacha ukatafute hiyo hela, haimfungi mtu. Kesi za madai sio kesi za jinai..sasa hapo imagine hapo ni wasanii wangapi leo unawafanyia kazi ya million 40 Million 50, ambayo ukiingia katika intellectual property court (mahakama ya maswala ya copy right), na copy right ni very expensive, tunaongelea six figures, eight figures. Sasa angalia ni wasanii wangapi hapa Tanzania wanaweza kukulipa eight figures.?” Amesema.
Kutokana na hali hiyo amesisitiza kuwa kuna haja ya kuwalipa wasanii pesa nyingi katika kazi zao huko wanakoenda kufanya ili wanapopata matatizo waweze kulipa, na kwamba bila hivyo mikataba ya label na wasanii Tanzania itakuwa useless.
Hii inamaanisha kuwa hakuna hatua zozote za kisheria ambazo B’hits itachukua kudai fidia kutoka kwa wasanii hao.
Hata hivyo uongozi wa B’Hits umesema utaachia nyimbo nyingine za wasanii hao zilizoko studio na kwamba zitachezwa redioni, lakini wasanii hao hawatakuwa na haki ya kuzitumia kwa kuwa ni mali halali ya kampuni hiyo.

Wednesday, November 13, 2013

Promoter DMK aeleza kwa nini wasanii wa hip hop Bongo hawapati shows Marekani kama waimbaji, awashauri cha kufanya

Promoter DMK aeleza kwa nini wasanii wa hip hop Bongo hawapati shows Marekani kama waimbaji, awashauri cha kufanya



Promoter DMK, mtanzania anayefanya kazi ya kuwapeleka wasanii wa Afrika nchini Marekani na kuwaleta wamarekani Afrika, amesema wasanii wa bongo wanaofanya hip hop wanapata changamoto zaidi ya nafasi ya kupiga shows Marekani kwa sababu ya lugha wanayotumia na kwamba kule kuna watu wengi wanaofanya hip hop halisi.

DMK ambaye pia anamiliki kituo cha radio na TV ‘Swahili radio&TV’ kilichoko Marekani,  amefunguka katika kipindi cha ‘The Jump Off’ cha 100.5 Times fm alipokuwa akipiga story na Jabir Saleh, Dj D_Ommy na Dj K_U kuhusu fursa za wasanii wa bongo kupiga shows Marekani kupitia kampuni yake ya ‘DMK Global’.

“We unakuja unaimba hip hop halafu unaimba Kiswahili, ujue inakuwa kazi kidogo kwa sababu kule watu wanaimba hip hop na wanafanya ile yenyewe, sasa wewe unakuja unaimba Kiswahili inakuwa inasumbua kidogo.” Alisema DMK.

Promoter huyo aliwashauri wasanii wa Hip Hop kitu cha kufanya ambacho kitawawezesha kupiga shows Marekani na kukubalika pia.

“Sisi tunajaribu kidogo kuwaambia hawa wanamuziki wa hapa wapige muziki ambao uko commercial kidogo, kwa sababu muziki ni business sasa kama muziki ni business inabidi wacommercialize muziki wao.” Alisema DMK.

Wednesday, August 7, 2013

LEGENDS DON'T SPEAK MUCH

Legends dont speak much cause we believe action speaks louder than words, come join the legends @isumba lounge (jollies club) this eid and dance to ur favourite tunes from the 80's to the late 90's, behind the 1 and 2 DJ John Dillinga aka the Legend is Back, DJ Fast Eddy and DJ Young Kelvin. Party starts on eid eve 2 the 2nd eid. Doors open 9pm, entry on the 1st eid 10k b4 mid midnight 15k after mid night dont miss it.

PETER OKOYE WA P SQUARE AVUNJA UKIMYA

Member wa kundi la P square Peter Okoye ameamua kuvunja ukimya kwa kumvisha pete ya uchumba mpenzi wa siku nyingi waliodumu kwenye uhusiano kwa miaka saba na mama watoto wake wawili Lola Omotayo. Peter ametumia aina tofauti na iliyozoeleka ya kuvishana pete kwa kum-suprise bi dada kwa gari jeupe la kifahari Range Rover jipya kabisa juu akaweka maua na peter ya uchumba! Cheki picha..

BEI YA MKAA (DJ K U EXT) - NIKKI WA PILI FT JOH MAKINI