Tuesday, July 17, 2012

CHEGE APATA AJALI



Hivi ndivyo gari la Chege lilivyokuwa baada ya ajali

Msanii wa Kigoma All Stars Chege Chigunda usiku wa jana amepata ajali mbaya ya gari maeneo ya Temeke jijini Dar es Salaam.

Taarifa za awali kuhusu ajali hiyo zimesema kuwa usiku huo Chege alikuwa ametokea jijini Nairobi.
 
Chege amesema usiku huo wa saa nne akiwa kwenye gari alikutana pikipiki katika mtaa mmoja wa maeneo ya Temeke ambaye alimgonga na yeye kupata ajali hiyo.

Chege amepata majeraha kadhaa lakini anaendelea vizuri licha ya gari lake kuharibika vibaya maeneo ya mbele.


Haikuweza kufahamika mara moja hali ya mtu huyo aliyekuwa na pikipiki.

NAHUU NI UJUMBE KUTOKA KWA CHEGE : habari jamani!taarifa zinazosambazwa sio nzuri!mimi nimepata ajali kubwa sana jana bt nashkuru nimepona kbs,jamaa wa bodaboda alikua amepora pikipiki ya watu,na alikua amelewa sana so baada ya ajali alivunjika mguu kbs na bodabaoda imekatika yote gari yangu pia imekufa kabisa bt namshkuru mungu uhai bado ninao!huo ndio ukweli kamili