Thursday, July 26, 2012

Serikali ya Tanzania itajaribu matibabu kwa njia ya mtandao (TeleMedicine)

Serikali imesema itaanzisha mradi wa majaribio wa matibabu kwa kwa njia ya mtandao (Telemedicine) kwa mwaka huu wa fedha ukishirikisha hospitali mbalimbali nchini.

Akisoma hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2012/13 ya Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu bungeni leo, Waziri wa Wizara hiyo, Profesa Makame Mbarawa alisema mpango huo utahusisha Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) na hospitali mbalimbali nchini.

Alitaja hospitali hizo zitakazounganishwa na mtandao huo wa matibabu kuwa ni Muhimbili, Amana, Temeke, Mwananyamala, Tumbi na Bagamoyo. Alisema mpango huo utafanyika kwa kuihusisha Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia na wadau wengine.