Sunday, August 12, 2012

NEW HIT: BAGHDAD FT AMIN - NIMEWASAMEHE


Track ; nimewasamehe

Artist  ; Baghdad ft  Amini

Studio ; Shine rec

Producer ; Mr t 

Project ; wajukuuu int

   Hii  ni ngoma iliyojko katika muendelezo wa project za msanii ambae awali alikuwa akiunda kundi la Mexicana lacavela ambao ndio wanaotazamiwa kuwa mahasimu wake wakubwa kwa kipindi hichi chote tangu Baghdad alipotangaza kujitoa Mexicana lacavela mwishoni mwa mwaka jana. Baghdad ; mimi nilikuwa kama pm (program manager ) na manager wangu wa sasa alikuwa kama manager baada ya meesen kuachia ngazi  na ndipo tuliamua kupanga mikakati ili kuipeperusha bendera ya Mexicana ila haikufanikiwa kwa kuwa baadhi ya wasanii waliokuwa wakiunda kundi hilo kuhisi wamefika safari yao. Baghdad aliamua kujitoa na kuamua kufanya project zake kama solo artist chini ya manager wa zamani wa mexaicana lacavela anaefahamika kama daudi lucas kwenye jina lililopo kwenye id yake. Hivyo maisha mengi aliyopitia aliamua kuyaweka kwenye wimbo wake mpya aliouachia tar 11 mwezi 1gust 2012  mwezi ambao amezaliwa mama yake mzazi, kaka yake, na manager wake ameuita mwezi wenye Baraka kwake na upendo ndio maana ameamaua kukaa both na kutunga nyimbo kwa ajili ya kuwasamnehe wote waliowahi kumkosea, Baghdad ; unajua aidea alinipa manager wangu ilikuwa ni chungu cha pili wakati tunafuturu akaniambia si vyema kufunga wakati una dukuduku moyoni  so wasamehe watu waliokukosea na ndipo niliamua kukaa na kutunga ngoma iliowasamehe wale waliowahi kunitishia kuniua, walionichukulia mademu wangu kipindi nasoma, walionisingizia mambo nisiyofanya, niliowalaza hom wakati wamefukuzwa kwao na hawana pakwenda nikawa nawapa chakula, kwa zaidi ya miezi mitatu, kunao wengine walionikera kipindi nafanya kazi clouds media group, na zaidi ni mtu ambae nimemsaidia kufanya studio yake ijulikane tangu inaanza mpaka hapa ilipofika ila akadiriki kumtaka msichana ambae na diriki kusema ni furaha yangu ya milele aitwae anitha. Nimeamua kuwasamehe wote. Wote kama kuna yeyote aliyewahi kunikosea iwe kwa kutenda, kwa kufanya, kwa kuwaza au kwa njia yoyote nimemsamehe. Aidha baghda ameeleza ya kuwa kwa sasa hana majibizano yeyote na mtu yeyote kwa sababu kashasahau yote yaliowahi kutokea kitambo now nawaza jinsi ya kukabiliana na wasanii wa kimataifa ambao natarajia kufanya kazi nao.  

"baghdad ft amin - nimewasamehe.mp3"